قال رَسُــول اللَّهِ ﷺ
Amesema Mtume wa Allah – swala na salamu za Allah zimfikie-:
إنَّ أحدڪـم لن يمــوتَ حتى يستكملَ رزقَه ، فلا تستبطِئُوا الرِّزقَ ، واتقــوا اللهَ أيها الناسُ ، وأَجمِلوا فـي الطَّلبِ ، خُذوا ما حلَّ ، ودَعوا ما حـَرُمَ .
Hakika mmoja wenu hatofariki mpaka akamilishe riziki yake, basi musiione kuchelewa (hiyo) riziki, na mcheni Allah enyi watu! na fanyeni vizuri kutafuta (riziki) chukueni kilichokuwa halali na acheni kilichokuwa haramu .
📚‘ السلسلة الصحيحة – الصفحة أو الرقم: ٢٠٩/٦
Maelezo:
Riziki imekadiriwa kila mtu itamfikia hata kama anaona imechelewa, ikiwa ni hivyo basi tosheka na halali na achana na haramu na wala usiwe na pupa juu ya kuitafuta dunia.